1
Yohana 16:33
Swahili Roehl Bible 1937
Haya nimewaambia, mpate kutengemana mwangu. Ulimwenguni mnayo maumivu; lakini tulieni mioyo! Mimi nimeushinda ulimwengu.*
Mampitaha
Mikaroka Yohana 16:33
2
Yohana 16:13
Lakini yule atakapokuja, yule Roho wa kweli, yeye atawaongoza, awapeleke penye yote yaliyo ya kweli. Kwani hatayasema maneno yake mwenyewe, ila atayasema, atakayoyasikia, awatangazie nayo yatakayokuja.
Mikaroka Yohana 16:13
3
Yohana 16:24
Mpaka leo hakuna, mliloliomba katika Jina langu. Ombeni! Ndipo, mtakapopewa, furaha yenu iwe imetimizwa yote!
Mikaroka Yohana 16:24
4
Yohana 16:7-8
Lakini mimi nawaambiani lililo la kweli: Inawafalia, mimi niende zangu. Kwani nisipokwenda zangu, mtuliza mioyo hatawajia. Lakini nitakapokwenda, nitamtuma kwenu. Naye atakapokuja atawaumbua wao wa ulimwengu kuwa wenye makosa wasio nalo la kujikania, wanaopaswa na kuhukumiwa.
Mikaroka Yohana 16:7-8
5
Yohana 16:22-23
Basi, nanyi sasa mnasikitika, lakini tutaonana tena, ndipo, mioyo yenu itakapofurahi; hiyo furaha yenu hakuna atakayeiondoa kwenu. Siku ile hamtaniuliza neno.* *Kweli kweli nawaambiani: Lo lote, mtakalomwomba Baba, atawapa katika Jina langu.
Mikaroka Yohana 16:22-23
6
Yohana 16:20
Kweli kweli nawaambiani: Ninyi mtalia na kuomboleza, lakini wao wa ulimwengu watafurahi. Ninyi mtasikitika, lakini sikitiko lenu litageuka kuwa furaha.
Mikaroka Yohana 16:20
Fidirana
Baiboly
Planina
Horonan-tsary