Zaburi 25

25
Kumwomba Mungu uongozi na ulinzi
(Zaburi ya Daudi)
1Ee Mwenyezi-Mungu, kwako naielekeza nafsi yangu!
2Nakutumainia wewe, ee Mungu wangu,
usiniache niaibike;
adui zangu wasifurahie kushindwa kwangu.
3Usimwache anayekutumainia apate aibu;
lakini waaibike wote wanaokuasi kwa makusudi.
4Unijulishe njia zako, ee Mwenyezi-Mungu;
unifundishe nifuate unayotaka.
5Uniongoze katika ukweli wako na kunifundisha,
kwani wewe ni Mungu, mwokozi wangu;
ninakutegemea wewe kila siku.
6Uikumbuke huruma yako ee Mwenyezi-Mungu;
uzikumbuke na fadhili zako kuu,
ambazo zimekuwako tangu kale.
7Usikumbuke dhambi na makosa ya ujana wangu;
unikumbuke kadiri ya fadhili zako,
kwa ajili ya wema wako, ee Mwenyezi-Mungu.
8Mwenyezi-Mungu ni mwema na mnyofu,
kwa hiyo huwafundisha wenye dhambi njia.
9Huwaongoza wanyenyekevu katika uadilifu;
naam, huwafundisha hao njia yake.
10Mwenyezi-Mungu hutenda kwa fadhili na uaminifu,
kwa wale wanaoshika agano lake na maamuzi yake.
11Kwa ajili ya jina lako, ee Mwenyezi-Mungu,
unisamehe kosa langu kwani ni kubwa.
12Kila mtu anayemcha Mwenyezi-Mungu,
Mwenyezi-Mungu atamfunza njia ya kufuata.
13Mtu wa namna hiyo atafanikiwa daima,
na wazawa wake watamiliki nchi.
14Mwenyezi-Mungu ni rafiki ya wale wamchao;
yeye huwajulisha hao agano lake.
15Namwangalia Mwenyezi-Mungu daima;
yeye atainasua miguu yangu mtegoni.
16Unielekee, ee Mungu, unionee huruma,
maana mimi ni mpweke na mnyonge.
17Uniondolee mahangaiko ya moyoni mwangu;
unitoe katika mashaka yangu.
18Uangalie mateso yangu na dhiki yangu;
unisamehe dhambi zangu zote.
19Angalia jinsi walivyo wengi maadui zangu;
ona jinsi wanavyonichukia kwa ukatili.
20Uyalinde maisha yangu, uniokoe;
nakimbilia usalama kwako,
usikubali niaibike.
21Wema na uadilifu vinihifadhi,
maana ninakutumainia wewe.
22Ee Mungu, uwaokoe watu wako, Israeli;
uwaokoe katika taabu zao zote.

選択箇所:

Zaburi 25: BHN

ハイライト

シェア

コピー

None

すべてのデバイスで、ハイライト箇所を保存したいですか? サインアップまたはサインインしてください。