Mwanzo 29
29
Yakobo anafika kwa Labani
1Yakobo aliendelea na safari yake, akafika katika inchi za watu wa upande wa mashariki. 2Siku moja akaona kisima katika mbuga, na kando yake makundi matatu ya kondoo wakipumzika. Kondoo walikuwa wanakunyweshwa kutoka kisima hicho kilichokuwa kimefunikwa kwa jiwe kubwa. 3Kwa kawaida, makundi yote ya kondoo yalipokusanyika, wachungaji walirudisha lile jiwe kwa pamoja toka kwenye kisima na kuwakunywesha kondoo. Halafu walifunika tena kisima kwa jiwe lile.
4Yakobo akawauliza wachungaji: “Wandugu zangu, mumetoka wapi?”
Wakamujibu: “Tumetoka Harani.” 5Naye akawauliza: “Munamufahamu Labani mwana wa Nahori?”
Wakamujibu: “Tunamufahamu.”
6Akaendelea kuwauliza: “Yuko muzima?”
Nao wakamujibu: “Yeye ni muzima; hata binti yake Rakeli, yule kule anakuja na kondoo wake!”
7Kisha Yakobo akawaambia: “Ninaona ingaliki muchana, na si wakati wa kuwakusanya kondoo pamoja. Basi, mukunyweshe kondoo maji, muende kuwachunga.”
8Lakini wao wakamwambia: “Hatuwezi kufanya hivyo mpaka makundi yote yakuwe yamekusanyika pamoja, jiwe limeviringishwa juu ya kisima, halafu tutakunywesha kondoo.”
9Yakobo alipokuwa bado anazungumuza na hao wachungaji, Rakeli akafika na kondoo wa baba yake, maana yeye ndiye aliyekuwa akiwachunga. 10Yakobo akamwona Rakeli, binti ya mujomba wake Labani. Akaona kondoo ambao vilevile ni wa mujomba wake. Akakwenda na kuliviringisha lile jiwe kwenye mudomo wa kisima. Akakunywesha maji kundi la mujomba wake. 11Kisha Yakobo akamubusu Rakeli na kulia kwa sauti. 12Akamujulisha Rakeli kwamba yeye ni wa jamaa ya baba yake, na kwamba ni mwana wa Rebeka.
Rakeli akakimbia mbio kwa nyumba akamwarifu baba yake. 13Labani aliposikia habari za mwipwa wake Yakobo, alikwenda mbio kumupokea, akamukumbatia, akamubusu, akamukaribisha ndani ya nyumba yake. Yakobo akamwelezea Labani mambo yote yaliyotokea. 14Naye Labani akasema: “Hakika, wewe ni jamaa yangu, damu moja nami!” Yakobo akakaa naye kwa muda wa mwezi mumoja.
Yakobo anaoa wabinti za Labani
15Siku moja Labani akamwambia Yakobo: “Wewe ni jamaa yangu lakini hiyo haisemi kwamba utanitumikia bure. Uniambie unataka mushahara gani!” 16Sasa, Labani alikuwa na wabinti wawili: mukubwa anayeitwa Lea na mudogo anayeitwa Rakeli. 17Lea alikuwa na macho zaifu, lakini Rakeli alikuwa muzuri na wa kupendeza.
18Yakobo akamupenda Rakeli; kwa hiyo akamwambia Labani: “Nitakutumikia miaka saba kwa ajili ya Rakeli, binti yako mudogo.”
19Labani akamwambia: “Afazali nimwoeshe Rakeli kwako wewe kuliko kumwoesha kwa mutu mwingine yeyote. Endelea kuishi nami.” 20Basi, Yakobo akamutumikia Labani miaka saba kwa ajili ya Rakeli, lakini kwake muda ule ulikuwa kama siku chache, kwa vile alivyomupenda Rakeli.
21Kisha Yakobo akamwambia Labani: “Muda wangu umetimia, kwa hiyo unipe muke wangu.” 22Basi, Labani akafanya karamu na kuwaalika watu wote wa kule. 23Lakini magaribi, Labani akatwaa Lea, binti yake mukubwa, na kumupeleka kwa Yakobo. Yakobo akalala naye. 24(Labani akamutoa Zilpa, mujakazi wake, akuwe mutumishi wa Lea.) 25Asubui, Yakobo akatambua kwamba ni Lea! Basi, akamwuliza Labani: “Umenitendea jambo gani? Si nilikutumikia kwa ajili ya Rakeli? Mbona basi, umenidanganya?”
26Labani akamujibu: “Katika inchi yetu hatufanyi hivyo. Si desturi yetu kumwoesha binti mudogo mbele ya mukubwa. 27Umutimizie Lea siku zake saba za ndoa, nasi tutakupa Rakeli kwa utumishi wa miaka saba mingine.”
28Yakobo akakubali. Na Yakobo alipomutimizia Lea siku zake saba, Labani akamupa Rakeli, binti yake mudogo akuwe muke wake. 29(Labani akamutoa Biliha, mujakazi wake, akuwe mujakazi wa Rakeli). 30Basi, Yakobo akalala na Rakeli vilevile. Lakini Yakobo akamupenda Rakeli kuliko Lea. Akamutumikia Labani miaka mingine saba.
Watoto wa Yakobo
31Yawe alipoona kwamba Lea anachukiwa, akamujalia watoto; lakini Rakeli alikuwa tasa. 32Lea akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume, akamwita Rubeni,#29.32 Rubeni: ni kama neno la Kiebrania lenye maana “Angalia, mwana” au: “Ameona taabu zangu”. akisema: “Yawe ameona mateso yangu; bila shaka sasa mume wangu atanipenda.” 33Lea akapata mimba tena, akazaa mutoto mwanaume, akamwita Simeoni,#29.33 Simeoni: ni kama neno la Kiebrania lenye maana “Sikia”. akisema: “Yawe amenipa mutoto mwingine mwanaume kwa sababu amesikia jinsi ninavyochukiwa.” 34Akapata mimba mara nyingine, akazaa mutoto mwanaume, akamwita Lawi,#29.34 Lawi: ni kama neno la Kiebrania lenye maana “Jiunga”. akisema: “Wakati huu mume wangu atajiunga nami, maana nimemuzalia watoto watatu wanaume.” 35Lea akapata mimba tena, akazaa mutoto mwanaume, akamwita Yuda,#29.35 Yuda: ni kama neno la Kiebrania lenye maana “Sifu”. akisema: “Mara hii nitamusifu Yawe.” Kisha Lea akaacha kuzaa.
Currently Selected:
Mwanzo 29: SWC02
Highlight
Share
Copy
![None](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2F58%2Fhttps%3A%2F%2Fweb-assets.youversion.com%2Fapp-icons%2Fen-GB.png&w=128&q=75)
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.