YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 85

85
Kuliombea fanaka taifa
(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Wakorahi)
1Ee Mwenyezi-Mungu,
umeifadhili nchi yako;
umemjalia Yakobo bahati nzuri tena.
2Umewasamehe watu wako kosa lao;
umezifuta dhambi zao zote.
3Umeizuia ghadhabu yako yote;
umeiacha hasira yako kali.
4Uturekebishe tena, ee Mungu mwokozi wetu;
uiondoe chuki uliyo nayo juu yetu.
5Je, utatukasirikia hata milele?
Je, utadumisha ghadhabu yako kwa vizazi vyote?
6Je, hutatujalia tena maisha mapya,
ili watu wako wafurahi kwa sababu yako?
7Utuoneshe, fadhili zako, ee Mwenyezi-Mungu,
utujalie wokovu wako.
8Hebu nisikie anachosema Mwenyezi-Mungu;
maana anaahidi kuwapa watu wake amani,
watu wake mwenyewe wasiporudia upuuzi wao
9Hakika yu tayari kuwaokoa wanaomheshimu,
na utukufu wake utadumu nchini mwetu.
10Fadhili zake na uaminifu vitakutana;
uadilifu na amani vitaungana.
11Uaminifu utachipuka katika nchi;
uadilifu utashuka toka mbinguni.
12Naam, Mwenyezi-Mungu atatuletea fanaka,
na nchi yetu itatoa mazao yake mengi.
13Uadilifu utamtangulia Mungu
na kumtayarishia njia yake.

Currently Selected:

Zaburi 85: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in