YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 58

58
Mungu hakimu wa mahakimu
(Kwa Mwimbishaji: Mtindo “Usiharibu”. Utenzi wa Daudi)
1Enyi watawala,#58:1 watawala; au Miungu. je, mwahukumu kwa haki kweli?
Je, mnawahukumu watu kwa adili?
2La! Nyinyi mwafikiria tu kutenda maovu;
nyinyi wenyewe mwaeneza dhuluma nchini.
3Waovu wamepotoka tangu kuzaliwa kwao,
waongo hao, wamekosa tangu walipozaliwa.
4Wana sumu kama sumu ya nyoka;
viziwi kama joka lizibalo masikio,
5ambalo halisikii hata sauti ya mlozi,
au utenzi wa mganga stadi wa uchawi.
6Ee Mungu, wavunje meno yao,
yangoe, ee Mwenyezi-Mungu, meno ya simba hao.
7Watoweke kama maji yanayodidimia mchangani,
kama nyasi wakanyagwe na kunyauka,
8watoweke kama konokono ayeyukavyo,
kama mimba iliyoharibika isiyoona kamwe jua!
9Kabla hawajatambua, wangolewe
kama miiba, michongoma au magugu.
Kwa hasira ya Mungu, wapeperushwe mbali,
wakiwa bado hai.
10Waadilifu watafurahi waonapo waovu wanaadhibiwa;
watatembea katika damu ya watu wabaya.
11Watu wote watasema: “Naam, waadilifu hupata tuzo!
Hakika yuko Mungu anayeihukumu dunia!”

Currently Selected:

Zaburi 58: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in