YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 48

48
Siyoni mji wa Mungu
(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Wakorahi)
1Mwenyezi-Mungu, ni mkuu; astahili kusifiwa sana
katika mji wake na mlima wake mtakatifu.
2 # Taz Mat 5:35 Mlima Siyoni huko kaskazini, wapendeza kwa urefu;
mji wa Mfalme mkuu ni furaha ya ulimwengu.
3Mungu anazilinda ngome zake;
yeye amejionesha kuwa ngome ya usalama.
4Wafalme walikusanyika,
wakaenda pamoja kushambulia.
5Lakini walipouona mji wa Siyoni, wakashangaa;
wakashikwa na hofu, wakatimua mbio.
6Hofu kuu iliwashika,
wakasikia uchungu kama mama anayejifungua,
7kama waliokumbwa na kimbunga cha mashariki
ambacho huzivunjavunja meli za Tarshishi.
8Yote tuliyosikia tumejionea wenyewe
katika mji wa Mwenyezi-Mungu wa majeshi,
naam, katika mji wa Mungu wetu;
Mungu atauimarisha milele.
9Ee Mungu, twazitafakari fadhili zako,
tukiwa hekaluni mwako.
10Jina lako lasifika kila mahali,
sifa zako zaenea popote duniani.
Kwa mkono wako umetenda kwa haki;
11watu wa Siyoni na wafurahi!
Watu wa Yuda na washangilie,
kwa sababu ya maamuzi yako ya haki!
12Tembeeni huko Siyoni mkauzunguke,
mkaihesabu minara yake.
13Zitazameni kuta zake
na kuchunguza ngome zake;
mpate kuvisimulia vizazi vijavyo, kwamba:
14“Huyu ni Mungu, Mungu wetu milele!
Atakuwa kiongozi wetu milele!”

Currently Selected:

Zaburi 48: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in