YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 4

4
Kuomba msaada jioni
(Kwa Mwimbishaji: Na ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi)
1Ee Mungu mtetezi wa haki yangu, unijibu niombapo.
Nilipokuwa katika shida, wewe ulinisaidia;
unionee huruma na kusikia sala yangu.
2Jamani, mtaniharibia jina langu mpaka lini?
Mpaka lini mtapenda upuuzi na kusema uongo?
3Jueni kuwa Mwenyezi-Mungu amejiteulia mwaminifu wake.
Mwenyezi-Mungu husikia kila ninapomwomba.
4 # Efe 4:26 Tetemekeni kwa hofu na msitende dhambi;
tafakarini vitandani mwenu na kunyamaza.
5Toeni tambiko zilizo sawa,
na kumtumainia Mwenyezi-Mungu.
6Wengi husema: “Laiti tungepata tena fanaka!
Utuangalie kwa wema, ee Mwenyezi-Mungu!”
7Lakini mimi umenijalia furaha kubwa moyoni,
kuliko ya hao walio na divai na ngano kwa wingi.
8Nalala na kupata usingizi kwa amani;
ee Mwenyezi-Mungu, wewe peke yako waniweka salama.

Currently Selected:

Zaburi 4: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in