YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 24

24
Mfalme Mkuu
(Zaburi ya Daudi)
1 # Taz 1Kor 10:26 Dunia na vyote vilivyomo ni vyake Mwenyezi-Mungu;
ulimwengu na wote waishio humo ni mali yake.
2Maana yeye aliweka misingi ya dunia juu ya bahari;
aliisimika imara juu ya mito ya maji.
3Nani atakayepanda mlima wa Mwenyezi-Mungu?
Nani atakayekaa katika hekalu lake takatifu?
4 # Taz Mat 5:8 Ni mtu wa matendo mema na moyo safi,
asiyeuelekeza moyo wake katika upuuzi,
wala kuapa kwa uongo.
5Mtu huyo atapokea baraka kwa Mwenyezi-Mungu,
na haki yake kwa Mungu mwokozi wake.
6Ndio hali ya kizazi cha watu wamtafutao yeye;
naam, watu wamtafutao Mungu wa Yakobo.
7Fungukeni enyi milango;
fungukeni enyi milango ya kale,
ili Mfalme mtukufu aingie.
8Ni nani huyo Mfalme mtukufu?
Ni Mwenyezi-Mungu, mwenye nguvu na uwezo;
Mwenyezi-Mungu, mwenye uwezo vitani.
9Fungukeni enyi malango,
fungukeni enyi milango ya kale,
ili Mfalme mtukufu aingie.
10Ni nani huyo Mfalme mtukufu?
Ni Mwenyezi-Mungu, wa majeshi,
yeye ndiye Mfalme mtukufu.

Currently Selected:

Zaburi 24: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy