YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 146

146
Sifa kwa Mungu Mwokozi
1Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Umsifu Mwenyezi-Mungu, ee nafsi yangu!
2Nitamsifu Mwenyezi-Mungu maisha yangu yote;
nitamwimbia Mungu wangu muda wote niishipo.
3Msiwategemee wakuu wa dunia;
hao ni binadamu tu, hawawezi kuokoa.
4Binadamu akitoa pumzi yake ya mwisho,
anarudi mavumbini alimotoka;
na hapo mipango yake yote hutoweka.
5Heri mtu anayesaidiwa na Mungu wa Yakobo,
mtu aliyeweka tumaini lake kwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wake,
6 # Taz Mate 4:24; 14:15 aliyeumba mbingu na dunia,
bahari na vyote vilivyomo.
Yeye hushika ahadi yake milele.
7Yeye huwapatia wanaoonewa haki zao,
huwapa wenye njaa chakula.
Mwenyezi-Mungu huwapa wafungwa uhuru,
8huwafungua macho vipofu.
Mwenyezi-Mungu huwainua waliokandamizwa;
huwapenda watu walio waadilifu.
9Mwenyezi-Mungu huwalinda wageni,
huwategemeza wajane na yatima;
lakini huipotosha njia ya waovu.
10Mwenyezi-Mungu atawala milele,
Mungu wako, ee Siyoni, ni mfalme vizazi vyote!
Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Currently Selected:

Zaburi 146: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in