YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 130

130
Kuomba msaada
(Wimbo wa Kwenda Juu)
1Toka upeo wa unyonge wangu,
nakulilia, ee Mwenyezi-Mungu.
2Ee Bwana, sikia sauti yangu,
uitegee sikio sauti ya ombi langu.
3Kama, ee Mwenyezi-Mungu ungekumbuka maovu yetu
nani, ee Bwana, angeweza kusalimika?
4Lakini kwako twapata msamaha,
ili sisi tukuheshimu.
5Namtumainia Mwenyezi-Mungu kwa moyo wangu wote;
nina imani sana na neno lake.
6Ninamtumainia Mwenyezi-Mungu
kuliko walinzi wanavyongojea pambazuko;
kuliko walinzi wanavyongojea kuche asubuhi.
7Ee Israeli, umtumainie Mwenyezi-Mungu,
maana kwake Mwenyezi-Mungu kuna fadhili,
kwake kuna nguvu kubwa ya kutukomboa.
8 # Taz Mat 1:21; Tito 2:14 Yeye atawakomboa watu wa Israeli
kutoka katika maovu yao yote.

Currently Selected:

Zaburi 130: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in