YouVersion Logo
Search Icon

Mwanzo 9

9
Mungu anafanya agano na Noa
1Mungu akamubariki Noa na wana wake, akiwaambia: “Muzae, muongezeke, mujaze inchi. 2Nyama wote, ndege wote wa anga, viumbe vyote vinavyotambaa juu ya inchi na samaki wote wa bahari watakuwa na hofu na kuwaogopa ninyi. Wote wamewekwa chini ya mamlaka yenu. 3Nyama wote wenye uzima watakuwa chakula chenu; ninawapa nyama hao kama vile nilivyowapa mimea kuwa chakula chenu. 4Lakini musikule nyama wenye damu, maana uzima uko katika damu. 5Damu ya uzima wenu nitaidai. Nitaidai kutoka kwa kila nyama na mwanadamu. Atakayemwua mwanadamu mwenzake, nitamudai uzima wake.
6Anayemwanga damu ya mwanadamu,
damu yake itamwangwa na mwanadamu;
maana mwanadamu aliumbwa kwa mufano wa Mungu.
7Nanyi muzae, mwongezeke,
muzae kwa wingi, mwongezeke katika inchi.”
Upinde wa mvua
8Kisha Mungu akamwambia Noa na wana wake: 9“Ninasimamisha agano langu nanyi na wazao wenu 10na viumbe vyote vyenye uzima, ndege, nyama wa kufugwa na wa pori, wote waliotoka katika chombo pamoja nanyi. 11Ninasimamisha agano langu nanyi, kwamba hakutatokea tena mafuriko ya maji kwa kuangamiza inchi nzima au viumbe vyote vyenye uzima.” 12Tena Mungu akasema: “Hiki ndicho kitambulisho cha agano ninalofanya kati yangu nanyi na kila kiumbe chenye uzima kinachokuwa pamoja nanyi kwa vizazi vyote vinavyokuja: 13ninaweka upinde wangu katika mawingu, nao utakuwa kitambulisho cha agano kati yangu na dunia. 14Kila mara nitakapofunika dunia kwa mawingu, na huo upinde wa mvua utakapoonekana katika mawingu, 15nitakumbuka agano langu nanyi na viumbe vyote vyenye uzima. Maji hayatageuka hata kidogo kuwa mafuriko ya kuangamiza viumbe vyote vyenye uzima. 16Huo upinde utakapotokea katika mawingu, nitauona na kukumbuka agano hilo la milele kati yangu na viumbe vyote vyenye uzima katika dunia.” 17Mungu akamwambia Noa: “Hiki ndicho kitambulisho cha agano ambalo nimesimamisha na viumbe vyote vyenye uzima katika dunia.”
Noa na wana wake
18Wana wa Noa waliotoka katika chombo walikuwa Semu, Hamu na Yafeti. Hamu alikuwa baba ya Kanana. 19Hao ndio wana watatu wa Noa na kutokana nao watu walienea katika dunia yote.
20Noa alikuwa mulimaji wa kwanza kupanda mizabibu. 21Akakunywa divai, akalewa, kisha akalala uchi ndani ya hema yake. 22Hamu, baba ya Kanana, akaona uchi wa baba yake, akatoka inje na kuwaambia wandugu zake wawili. 23Lakini Semu na Yafeti wakatwaa nguo, wakaiweka juu ya mabega yao, wakakwenda kinyumenyume na kufunika uchi wa baba yao. Waliangalia pembeni, wala hawakuuona uchi wa baba yao. 24Ulevi wa Noa ulipokwisha naye alipojua alivyotendewa na mwana wake mudogo, 25akasema:
“Kanana alaaniwe!
Atakuwa mutumwa wa watumwa kwa wandugu zake.”
26Tena akasema:
“Semu abarikiwe na Yawe, Mungu wangu!#9.26 Semu Mungu wangu! au: Yawe, Mungu wa Semu, atukuzwe!
Kanana akuwe mutumwa wake.
27Mungu amuzidishe Yafeti,
aishi katika hema za Semu;
Kanana akuwe mutumwa wake.”
28Nyuma ya mafuriko ya maji, Noa aliishi miaka mia tatu na makumi tano, 29kisha akakufa akiwa na umri wa miaka mia tisa na makumi tano.

Currently Selected:

Mwanzo 9: SWC02

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in