YouVersion Logo
Search Icon

Mwanzo 6:1-4

Mwanzo 6:1-4 SWC02

Wakati watu walipoanza kuongezeka katika dunia na kuzaa wabinti, wana wa Mungu wakaona kwamba wale wabinti za watu ni wazuri, wakawatwaa wale waliowapendeza kuwa wake zao. Kwa hiyo, Yawe akasema: “Roho yangu haitakaa ndani ya wanadamu milele, maana yeye ni wa kufa tu. Basi, hataishi zaidi ya miaka mia moja na makumi mbili.” Katika siku zile na hata kisha, kulikuwa majitu katika dunia ambao walikuwa wazao wa wana wa Mungu na wabinti za wanadamu. Hao ndio watu waliokuwa mashujaa na wenye sifa wa zamani, na waliitwa Wanefili.