YouVersion Logo
Search Icon

Mwanzo 38

38
Yuda na Tamari
1Wakati ule, Yuda akatengana na wandugu zake, akakwenda kukaa na mutu mumoja Mwadulami, jina lake Hira. 2Akiwa kule, Yuda akamwona binti ya Sua Mukanana, akamwoa. 3Binti ya Sua akapata mimba akazaa mutoto mwanaume, akamwita Eri. 4Akapata mimba ingine, akazaa mutoto mwanaume, akamwita Onani. 5Kisha akapata mutoto mwingine mwanamuke, akamwita Sela. Wakati Sela alipozaliwa, Yuda alikuwa Kezibu.
6Yuda alimwoea mutoto wake wa kwanza Eri mwanamuke anayeitwa Tamari. 7Lakini Eri, muzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu mbele ya Yawe, hivyo Yawe akamwua.
8Basi, Yuda akamwambia Onani: “Umutwae muke wa ndugu yako marehemu, maana vile ndivyo inavyokupasa kufanya, upate kumuzalia ndugu yako watoto.”
9Lakini Onani alijua kwamba hao watoto hawangekuwa wake. Kwa hiyo, alipolala na muke wa ndugu yake, alimwanga chini mbegu ya uzazi, kusudi asimupatie ndugu yake watoto. 10Tendo hilo likamwuzi Yawe, akamwua Onani vilevile.
11Halafu Yuda akamwambia Tamari, muke wa mwana wake: “Rudi kwa nyumba ya baba yako, ubaki mujane mpaka wakati mwana wangu Sela atakapokomaa.” Yuda hakutaka Sela naye akufe kama vile wandugu zake. Basi, Tamari akarudi kwa nyumba ya baba yake.
12Nyuma ya muda, binti ya Sua, muke wa Yuda, akakufa. Yuda alipomaliza kufanya kilio akaondoka na rafiki yake Hira Mwadulami, wakakwenda Timuna kwa kukata manyoya ya kondoo wake. 13Tamari aliposikia kwamba baba mukwe wake alikuwa katika njia kwenda Timuna kukata manyoya ya kondoo wake, 14akavua nguo zake za ujane na kujifunika kitambaa. Kisha akaikaa kwenye mulango wa kuingilia Enaimu, kijiji kilichokuwa katika njia kwenda Timuna. Alifanya hivyo kwa vile aliona kwamba Sela alikwisha kuwa mutu muzima, lakini yeye Tamari hakuoeshwa akuwe muke wake.
15Basi, Yuda alipokuta Tamari pale, alimuzania kuwa mwanamuke kahaba, maana alikuwa akijifunika uso. 16Halafu, bila kujua kwamba huyo alikuwa muke wa mwana wake, akamwendea pale kando ya njia, akamwambia: “Ninataka kulala nawe.”
Tamari akamwuliza: “Utanipa nini upate kulala nami?”
17Yuda akamujibu: “Nitakupa mwana-mbuzi kutoka kundi langu.”
Tamari akamwambia: “Weka rehani kwa kuhakikisha kwamba utaniletea yule mwana-mbuzi.”
18Yuda akamwuliza: “Unataka nikupe nini kama rehani?”
Naye akamujibu: “Unipe hiyo pete na kamba yake pamoja na hiyo fimbo unayoshika.” Basi, Yuda akamupa vitu hivyo vyote, akalala naye. Tamari akapata mimba yake. 19Basi, Tamari akarudi kwa nyumba akavua kile kitambaa alichojifunika, akavaa tena nguo zake za ujane.
20Wakati Yuda alipomutuma yule rafiki yake, Mwadulami, amupelekee yule mwanamuke mwana-mbuzi kusudi arudishiwe rehani aliyomwachia, Hira hakumupata. 21Hira akauliza wenyeji wa Enaimu: “Yuko wapi yule mwanamuke kahaba aliyekuwa kando ya njia karibu na hapa?”
Wakamujibu: “Hapa hapajakuwa mwanamuke kahaba.”
22Basi, huyo rafiki akarudi kwa Yuda, akamwambia: “Sikumupata! Tena wenyeji wa kule wameniambia kwamba hapajakuwa mwanamuke kahaba yeyote kule.”
23Yuda akasema: “Acha avichukue vitu hivyo. Kama sivyo atatufanya tuchekelewe. Wewe mwenyewe umeona kwamba nilimupelekea mwana-mbuzi, lakini wewe haukumupata.”
24Kisha miezi mitatu, Yuda akapata habari hii: “Tamari, muke wa mwana wako amekuwa kahaba, tena amepata mimba kwa kufanya ukahaba.”
Basi, Yuda akaamuru: “Mumutoshe inje achomwe kwa moto!”
25Walipokuwa wakimutoa inje, Tamari akatuma ujumbe kwa baba mukwe wake, akisema: “Mwenye vitu hivi ndiye aliyenipa mimba. Kwa hiyo, ninakuomba umutambue mwenye pete hii na kamba yake, na fimbo hii.”
26Yuda akavitambua vitu hivyo, akasema: “Tamari ni mwenye haki kuliko mimi. Ni kweli, maana sikumwoesha kwa mwana wangu Sela.” Tokea siku hiyo Yuda hakulala tena na Tamari.
27Wakati wa kuzaa kwa Tamari ulipofika, ikafahamika kwamba alikuwa na mimba ya mapacha. 28Basi, alipopata uchungu wa kuzaa, pacha mumoja akatoa mukono inje, naye muzalishaji akaufunga kwa uzi mwekundu, akisema: “Huyu ndiye aliyezaliwa kwanza.” 29Lakini yule mutoto alipourudisha mukono wake ndani, ndugu yake akazaliwa wa kwanza. Muzalishaji akasema: “Mbona wewe umepita kwa nguvu?” Kwa hiyo akaitwa Peresi.#38.29 Peresi: Kiebrania maana yake “kutoka kwa nguvu”. 30Kisha ndugu yake akazaliwa akiwa na ule uzi mwekundu kwenye mukono, naye akaitwa Zera.#38.30 Zera: ni kama neno la Kiebrania lenye maana “nuru nyekundu ya mapambazuko”.

Currently Selected:

Mwanzo 38: SWC02

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in