YouVersion Logo
Search Icon

Mwanzo 36

36
Wazao wa Esau
(1 Sik 1.34-37)
1Hawa ndio wazao wa Esau ni kusema Edomu. 2Esau alioa wake Wakanaa: Ada binti ya Eloni Muhiti, Oholibama binti ya Ana, binti ya Sibeoni Muhivi, 3na Basemati binti ya Isimaeli, dada ya Nebayoti. 4Ada alimuzalia Esau Elifazi, naye Basemati akamuzalia Reueli. 5Oholibama alimuzalia Yeusi, Yalamu na Kora. Hao ndio wana wa Esau ambao wake zake walimuzalia alipokaa katika inchi ya Kanana.
6Kisha, Esau akawatwaa wake zake, watoto wake wanaume na wanawake, watu wote wa nyumba yake, ngombe wake, nyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata katika inchi ya Kanana, akahamia pahali pengine, mbali na ndugu yake Yakobo. 7Alifanya hivyo kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi hata wasiweze kuishi pamoja. Inchi walimokaa kama wageni haikuweza kuwatoshelea kwa sababu ya wingi wa nyama wao. 8Kwa hiyo, Esau akakwenda kukaa katika inchi ya milima ya Seiri. Jina lingine la Esau ni Edomu.
9Hawa ndio wazao wa Esau, baba ya Waedomu katika inchi ya milima ya Seiri. 10Wana wa Esau walikuwa Elifazi aliyezaliwa na Ada muke wake, na Reueli aliyezaliwa na Basemati muke wake mwingine. 11Wana wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi. 12Elifazi alikuwa na habara, jina lake Timuna. Huyu alimuzalia mwana, jina lake Amaleki. 13Basemati, muke wa Esau, alizaa Reueli. Wana wa Reueli walikuwa Nahati, Zera, Sama na Miza. 14Oholibama, binti ya Ana, binti ya Sibeoni, alimuzalia Esau mume wake wana watatu: Yeusi, Yalamu na Kora.
15Hawa ndio wakubwa wa makabila yaliyotokana na Esau. Elifazi, aliyekuwa muzaliwa wa kwanza wa Esau alizaa Temani, Omari, Sefo, Kenazi, 16Kora, Gatamu na Amaleki. Kila mumoja wao akiwa mukubwa wa kabila lake. Hao wote ni wana wa Elifazi katika inchi ya Edomu, waliotokana na Ada, muke wa Esau.
17Reueli mwana wa Esau, alizaa Nahati, Zera, Sama na Miza. Kila mumoja wao akiwa mukubwa wa kabila lake. Hao wote ni wana wa Reueli katika inchi ya Edomu, waliotokana na Basemati, muke wa Esau.
18Wana wa Oholibama, muke wa Esau, walikuwa Yeusi, Yalamu na Kora. Kila mumoja wao akiwa mukubwa wa kabila lake. Hao wote ni wana wa Oholibama, binti ya Ana, muke wa Esau. 19Basi, hao ndio wazao wa Esau, maana yake Edomu. Kila mumoja wao akiwa mukubwa wa kabila lake.
Wazao wa Seiri
(1 Sik 1.38-42)
20Hawa ndio wazao wa Seiri, Muhori, na ndio wenyeji wa inchi hiyo: Lotani, Sobali, Sibeoni, Ana, 21Disoni, Eseri na Disani; kila mumoja wao akiwa mukubwa wa kabila lake kati ya Wahori wa uzao wa Seiri, katika inchi ya Edomu.
22Wana wa Lotani walikuwa Hori na Hemani; na dada ya Lotani aliitwa Timuna.
23Wana wa Sobali walikuwa Alwani, Manahati, Ebali, Sefo na Onamu.
24Wana wa Sibeoni walikuwa Aya na Ana. Ana ndiye aliyeona chemichemi za maji ya moto katika jangwa, alipokuwa anachunga punda wa baba yake Sibeoni. 25Watoto wa Ana walikuwa Disoni na binti mumoja jina lake Oholibama. 26Wana wa Disoni walikuwa Hemudani, Esibani, Itirani na Kerani.
27Wana wa Eseri walikuwa Bilihani, Zawani, na Akani.
28Wana wa Disani walikuwa Usi na Arani.
29Basi, hao ndio wakubwa wa Wahori: Lotani, Sobali, Sibeoni, Ana, 30Disoni, Eseri na Disani; kila mumoja wao akiwa mukubwa wa kabila lake katika inchi ya Seiri.
Wafalme wa inchi ya Edomu
(1 Sik 1.43-54)
31Hawa ndio wafalme waliotawala katika inchi ya Edomu, mbele mufalme yeyote hajawatawala Waisraeli: 32Bela mwana wa Beori alitawala inchi ya Edomu akiwa na makao yake makubwa katika muji wa Dinihaba. 33Bela alipokufa, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosira akatawala pahali pake. 34Yobabu alipokufa, Husamu wa inchi ya Watemani, akatawala pahali pake. 35Husamu alipokufa, Hadadi mwana wa Bedadi akatawala pahali pake, makao yake makubwa yakiwa katika muji wa Awiti. Huyu ndiye aliyewapiga na kuwashinda Wamidiani katika inchi ya Moabu. 36Hadadi alipokufa, Samula kutoka Masireka, akatawala pahali pake. 37Samula alipokufa, Sauli kutoka Rehoboti, muji unaokuwa karibu na muto Furati, akatawala pahali pake. 38Sauli alipokufa, Bali-Hanani mwana wa Akibori, akatawala pahali pake. 39Bali-Hanani mwana wa Akibori alipokufa, Hadari akatawala pahali pake, na jina la muji wake likiwa Pau. Muke wa Akibori alikuwa Mehetabeli, binti ya Matiredi, binti ya Mezahaba.
40Wakubwa wa makabila yaliyotokana na Esau kadiri ya makabila yao na makao yao walikuwa: Timuna, Alwa, Yeteti, 41Oholibama, Ela, Pinoni, 42Kenazi, Temani, Mibusari, 43Magdieli na Iramu. Hao ndio wakubwa wa makabila yaliyotokana na Edomu, maana yake, Esau, baba ya Edomu. Wametajwa kulingana na makao yao katika sehemu za inchi walizorizi.

Currently Selected:

Mwanzo 36: SWC02

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in