YouVersion Logo
Search Icon

Zab 136

136
Uumbaji wa Mungu na Matukio ya Kihistoria
1 # 1 Nya 16:34; 2 Nya 5:13; 7:3; Ezr 3:11; Zab 100:5; 106:1; 107:1; 118:1; Yer 33:11 Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
2 # Kut 18:11; Kum 10:17 Mshukuruni Mungu wa miungu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
3 # 1 Tim 6:15; Ufu 17:14 Mshukuruni Bwana wa mabwana;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
4Yeye peke yake afanya maajabu makuu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
5 # Mwa 1:1; Mit 3:19 Yeye aliyefanya mbingu kwa fahamu zake;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
6 # Mwa 1:2; Yer 10:12 Yeye aliyeitandaza nchi juu ya maji;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
7 # Mwa 1:16; Kum 4:19 Yeye aliyefanya mianga mikubwa;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
8Jua litawale mchana;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
9Mwezi na nyota zitawale usiku;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
10 # Kut 12:29 Yeye aliyewapiga Wamisri kwa kuwaua wazaliwa wa kwanza wao;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
11 # Kut 12:51 Akawatoa Waisraeli katikati yao;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
12Kwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
13 # Zab 78:13; Kut 14:21-29 Yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
14Akawavusha Israeli katikati yake;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
15Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
16 # Kum 8:15 Yeye aliyewaongoza watu wake jangwani;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
17Yeye aliyewapiga wafalme wakuu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
18 # Kum 29:7 Akawaua wafalme mashuhuri;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
19 # Hes 21:21-30 Sihoni, mfalme wa Waamori;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
20 # Hes 21:31-35 Na Ogu, mfalme wa Bashani;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
21 # Yos 12:1 Akaitoa nchi yao iwe urithi;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
22Urithi wa Israeli mtumishi wake;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
23 # Mwa 8:1; Kum 32:36; Zab 102:17; Isa 63:9; Lk 1:48 Aliyetukumbuka katika unyonge wetu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
24Akatuokoa na watesi wetu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
25 # Zab 104:27 Kila chenye mwili akipa chakula chake;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
26Mshukuruni Mungu wa mbingu;
Kwa maana fadhili zake ni za milele.

Currently Selected:

Zab 136: SUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy