YouVersion Logo
Search Icon

Mit 15

15
1Jawabu la upole hugeuza hasira;
Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.
2Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri;
Bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu.
3 # 2 Nya 16:9; Ayu 34:21; Mit 5:21; Yer 16:17; Zek 4:10; Ebr 4:13 Macho ya BWANA yako kila mahali;
Yakimchunguza mbaya na mwema.
4Ulimi safi ni mti wa uzima;
Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo.
5Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye;
Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.
6Katika nyumba ya mwenye haki mna akiba nyingi;
Bali mapato ya mtu mbaya huwa taabu tu.
7Midomo ya mwenye haki hueneza maarifa;
Bali moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.
8 # Isa 61:8; Yer 6:20; Amo 5:22; Lk 18:11 Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA;
Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake.
9 # Mit 21:21; Isa 51:1,7; 1 Tim 6:11 Njia ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA;
Bali humpenda mtu afuatiaye wema.
10Adhabu kali ina yeye aiachaye njia;
Naye achukiaye kukemewa atakufa.
11 # Yn 2:24; Mdo 1:24 Kuzimu na Uharibifu vi wazi mbele za BWANA;
Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu?
12Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa;
Wala yeye hawaendei wenye hekima.
13Moyo wa furaha huchangamsha uso;
Bali kwa huzuni ya moyo roho hupondeka.
14Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa;
Bali kinywa cha wapumbavu hula upumbavu.
15Siku zote za mtu ateswaye ni mbaya;
Bali ukunjufu wa moyo ni karamu ya daima.
16 # Mit 16:8; Mhu 4:6; 1 Tim 6:6 Kuwa na mali chache pamoja na kumcha BWANA;
Ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu.
17Chakula cha mboga penye mapendano;
Ni bora kuliko ng’ombe aliyenona pamoja na kuchukiana.
18Mtu wa hasira huchochea ugomvi;
Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.
19Njia ya mtu mvivu ni kama boma la miiba;
Bali mapito yao wenye unyofu hufanyika njia kuu.
20Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye;
Bali mpumbavu humdharau mamaye.
21 # Efe 5:15 Upumbavu ni furaha kwake aliyepungukiwa na akili;
Bali mwenye ufahamu huunyosha mwenendo wake.
22Pasipo mashauri makusudi hubatilika;
Bali kwa wingi wa washauri huthibithika.
23Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake;
Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!
24 # Flp 3:20 Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu;
Ili atoke katika kuzimu chini.
25BWANA ataing’oa nyumba ya mwenye kiburi;
Bali atauthibitisha mpaka wa mjane.
26Mashauri mabaya ni chukizo kwa BWANA;
Bali maneno yapendezayo ni safi.
27 # Yos 6:18; 1 Sam 8:3; Mit 1:19; Isa 5:8; Zek 5:3 Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe;
Bali achukiaye zawadi ataishi.
28 # 1 Pet 3:15 Moyo wa mwenye haki hufikiri jinsi atakavyojibu;
Bali kinywa cha wasio haki humwaga mabaya.
29 # Efe 2:12; Zab 34:15,16; Yn 9:31; Rum 8:26 BWANA yu mbali na wasio haki;
Bali huisikia sala ya mwenye haki.
30Mng’ao wa macho huufurahisha moyo;
Habari njema huinenepesha mifupa.
31Sikio lisikilizalo lawama yenye uhai
Litakaa kati yao wenye hekima.
32Akataaye maonyo huidharau nafsi yake mwenyewe;
Bali yeye asikilizaye lawama hujipatia ufahamu.
33Kumcha BWANA ni maonyo ya hekima;
Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.

Currently Selected:

Mit 15: SUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy