YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 82

82
Zaburi 82
Maombi Kwa Ajili Ya Kutaka Haki
Zaburi ya Asafu.
1 Mungu anaongoza kusanyiko kuu,
anatoa hukumu miongoni mwa “miungu”:
2 “Hata lini utaendelea kuwatetea wasio haki
na kuonyesha upendeleo kwa waovu?
3 Teteeni wanyonge na yatima,
tunzeni haki za maskini na walioonewa.
4Mwokoeni mnyonge na mhitaji,
wakomboeni kutoka mkononi mwa mwovu.
5 “Hawajui lolote, hawaelewi lolote.
Wanatembea gizani;
misingi yote ya dunia imetikisika.
6 “Nilisema, ‘Ninyi ni “miungu”;
ninyi nyote ni wana wa Aliye Juu Sana.’
7 Lakini mtakufa kama wanadamu wa kawaida;
mtaanguka kama mtawala mwingine yeyote.”
8 Ee Mungu, inuka uihukumu nchi,
kwa kuwa mataifa yote ni urithi wako.

Currently Selected:

Zaburi 82: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in