YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 75

75
Zaburi 75
Mungu Ni Mwamuzi
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo.
1 Ee Mungu, tunakushukuru,
tunakushukuru wewe,
kwa kuwa jina lako li karibu;
watu husimulia matendo yako ya ajabu.
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum;
ni mimi nihukumuye kwa haki.
3 Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka,
ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema,
‘Msijisifu tena,’
kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu;
msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’ ”
6Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi
au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye:
Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe
kilichojaa mvinyo unaotoka povu
uliochanganywa na vikolezo;
huumimina, nao waovu wote wa dunia
hunywa mpaka tone la mwisho.
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele;
nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote,
bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.

Currently Selected:

Zaburi 75: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in