YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 52

52
Zaburi 52
Hukumu Ya Mungu
Kwa mwimbishaji. Utenzi wa Daudi. Baada ya Doegi, Mwedomu kumwendea Sauli na kumjulisha kuwa: “Daudi amekwenda nyumbani kwa Ahimeleki.”
1 Ewe jitu, mbona unajivunia ubaya?
Kwa nini unajivuna mchana kutwa,
wewe ambaye ni fedheha mbele za Mungu?
2 Ulimi wako hupanga mashauri mabaya ya maangamizi.
Ni kama wembe mkali, ninyi mfanyao hila.
3 Unapenda mabaya kuliko mema,
uongo kuliko kusema kweli.
4 Unapenda kila neno lenye kudhuru,
ewe ulimi wenye hila!
5 Hakika Mungu atakushusha chini
kwa maangamizi ya milele:
atakunyakua na kukuondoa kwa nguvu
kutoka hema yako,
atakungʼoa kutoka nchi ya walio hai.
6 Wenye haki wataona na kuogopa,
watamcheka, wakisema,
7 “Huyu ni yule mtu ambaye
hakumfanya Mungu kuwa ngome yake,
bali alitumainia wingi wa utajiri wake,
na akawa hodari kwa kuwaangamiza wengine!”
Neema Ya Mungu
8 Lakini mimi ni kama mti wa mzeituni
unaostawi katika nyumba ya Mungu,
nautegemea upendo wa Mungu usiokoma
milele na milele.
9 Nitakusifu milele kwa yale uliyoyatenda,
nitatumaini jina lako, kwa kuwa jina lako ni jema.
Nitakusifu mbele ya watakatifu wako.

Currently Selected:

Zaburi 52: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in