YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 130

130
Zaburi 130
Kuomba Msaada
Wimbo wa kwenda juu.
1 Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu.
Masikio yako na yawe masikivu
kwa kilio changu unihurumie.
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi,
Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
4 Lakini kwako kuna msamaha,
kwa hiyo wewe unaogopwa.
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea,
katika neno lake naweka tumaini langu.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana
kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi,
naam, kuliko walinzi
waingojeavyo asubuhi.
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana,
maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma,
na kwake kuna ukombozi kamili.
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli
kutoka dhambi zao zote.

Currently Selected:

Zaburi 130: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in