YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 128

128
Zaburi 128
Thawabu Ya Kumtii Bwana
Wimbo wa kwenda juu.
1 Heri ni wale wote wamchao Bwana,
waendao katika njia zake.
2 Utakula matunda ya kazi yako;
baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao
ndani ya nyumba yako;
wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni
kuizunguka meza yako.
4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa
mtu amchaye Bwana.
5 Bwana na akubariki kutoka Sayuni
siku zote za maisha yako,
na uone mafanikio ya Yerusalemu,
6 nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako.
Amani iwe juu ya Israeli.

Currently Selected:

Zaburi 128: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in