Watu wale wote walipobatizwa, Yesu akabatizwa vilevile. Alipokuwa akiomba, mbingu zikafunguka, na Roho Mutakatifu akashuka juu yake katika hali ya kimwili kwa mufano wa njiwa. Na sauti ikasikilika toka mbinguni ikisema: “Wewe ndiwe Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa nawe sana.”