Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 103:6-22

Zaburi 103:6-22 Neno: Maandiko Matakatifu 2024 (NENO)

Mwenyezi Mungu hutenda haki, naye huwapa hukumu ya haki wote wanaodhulumiwa. Alimjulisha Musa njia zake, na watu wa Israeli matendo yake. Mwenyezi Mungu ni mwingi wa huruma na mwenye neema; si mwepesi wa hasira, bali amejaa upendo. Yeye hatalaumu siku zote, wala haweki hasira yake milele, yeye hatutendei kulingana na dhambi zetu wala hatupatilizi kwa kadiri ya maovu yetu. Kama vile mbingu zilivyo juu ya dunia, ndivyo wema wake ulivyo mwingi kwa wanaomcha; kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, ndivyo Mungu alivyoziweka dhambi zetu mbali nasi. Kama baba alivyo na huruma kwa watoto wake, ndivyo Mwenyezi Mungu anavyowahurumia wale wanaomcha; kwa kuwa anajua tulivyoumbwa, anakumbuka kwamba sisi tu mavumbi. Kuhusu mwanadamu, siku zake ni kama majani, anachanua kama ua la kondeni; upepo huvuma juu yake nalo hutoweka, mahali pake hapalikumbuki tena. Lakini kutoka milele hata milele upendo wa Mwenyezi Mungu uko kwa wale wamchao, nayo haki yake kwa watoto wa watoto wao: kwa wale walishikao agano lake na kukumbuka kuyatii mausia yake. Mwenyezi Mungu ameweka imara kiti chake cha enzi mbinguni, na ufalme wake unatawala vitu vyote. Mhimidini Mwenyezi Mungu, enyi malaika wake, ninyi mlio mashujaa, mnaozitii amri zake, ninyi mnaotii neno lake. Mhimidini Mwenyezi Mungu, ninyi jeshi lake lote la mbinguni, ninyi watumishi wake mnaofanya mapenzi yake. Mhimidini Mwenyezi Mungu, enyi kazi zake zote kila mahali katika milki yake.

Shirikisha
Soma Zaburi 103

Zaburi 103:6-22 Neno: Maandiko Matakatifu 2024 (NENO)

Mwenyezi Mungu hutenda haki, naye huwapa hukumu ya haki wote wanaodhulumiwa. Alimjulisha Musa njia zake, na watu wa Israeli matendo yake. Mwenyezi Mungu ni mwingi wa huruma na mwenye neema; si mwepesi wa hasira, bali amejaa upendo. Yeye hatalaumu siku zote, wala haweki hasira yake milele, yeye hatutendei kulingana na dhambi zetu wala hatupatilizi kwa kadiri ya maovu yetu. Kama vile mbingu zilivyo juu ya dunia, ndivyo wema wake ulivyo mwingi kwa wanaomcha; kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, ndivyo Mungu alivyoziweka dhambi zetu mbali nasi. Kama baba alivyo na huruma kwa watoto wake, ndivyo Mwenyezi Mungu anavyowahurumia wale wanaomcha; kwa kuwa anajua tulivyoumbwa, anakumbuka kwamba sisi tu mavumbi. Kuhusu mwanadamu, siku zake ni kama majani, anachanua kama ua la kondeni; upepo huvuma juu yake nalo hutoweka, mahali pake hapalikumbuki tena. Lakini kutoka milele hata milele upendo wa Mwenyezi Mungu uko kwa wale wamchao, nayo haki yake kwa watoto wa watoto wao: kwa wale walishikao agano lake na kukumbuka kuyatii mausia yake. Mwenyezi Mungu ameweka imara kiti chake cha enzi mbinguni, na ufalme wake unatawala vitu vyote. Mhimidini Mwenyezi Mungu, enyi malaika wake, ninyi mlio mashujaa, mnaozitii amri zake, ninyi mnaotii neno lake. Mhimidini Mwenyezi Mungu, ninyi jeshi lake lote la mbinguni, ninyi watumishi wake mnaofanya mapenzi yake. Mhimidini Mwenyezi Mungu, enyi kazi zake zote kila mahali katika milki yake.

Shirikisha
Soma Zaburi 103