Kumbukumbu la Sheria 6:13-15
Kumbukumbu la Sheria 6:13-15 Biblia Habari Njema (BHN)
Mtamcha Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, mtamtumikia yeye peke yake na kuapa kwa jina lake peke yake. Msiabudu miungu mingine, miungu ya watu walio jirani nanyi, hasira ya Mwenyezi-Mungu isije ikawaka juu yenu, naye akawafutilia mbali kutoka duniani, maana Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu aliye kati yenu, ni Mungu mwenye wivu.
Kumbukumbu la Sheria 6:13-15 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Mche BWANA, Mungu wako; ndiye utakayemtumikia, na kuapa kwa jina lake. Msifuate miungu mingine katika miungu ya mataifa wawazungukao; kwani BWANA, Mungu wako, aliye katikati yako ni Mungu mwenye wivu; isije ikawaka juu yako hasira ya BWANA, Mungu wako, akakuangamiza kutoka juu ya uso wa nchi.
Kumbukumbu la Sheria 6:13-15 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Mche BWANA, Mungu wako; ndiye utakayemtumikia, na kuapa kwa jina lake. Msifuate miungu mingine katika miungu ya mataifa wawazungukao; kwani BWANA, Mungu wako, aliye katikati yako ni Mungu mwenye wivu; isije ikawaka juu yako hasira ya BWANA, Mungu wako, akakuangamiza kutoka juu ya uso wa nchi.
Kumbukumbu la Sheria 6:13-15 Neno: Bibilia Takatifu (NEN)
Utamcha BWANA Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake na kuapa kwa jina lake. Usifuate miungu mingine, miungu ya mataifa yanayokuzunguka; kwa kuwa BWANA Mungu wako, ambaye yuko katikati yako, ni Mungu mwenye wivu na hasira yake itawaka dhidi yako, naye atakuangamiza kutoka uso wa nchi.