Luka 14:28-30
Luka 14:28-30 SRB37
Maana kwenu yuko mtu anayetaka kujenga mnara, asiyekaa kwanza na kuzihesabu shilingi za jengo, kama anazo za kulitimiza? Kwani akiisha kuweka msingi, asipoweza kumaliza, halafu wote wanaoviona wataanza kumfyoza wakisema: Mtu huyu alianza kujenga, naye hakuweza kumaliza.