Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 119:97-104

Zaburi 119:97-104 SRUV

Sheria yako naipenda mno ajabu, Ndiyo kutafakari kwangu mchana kutwa. Maagizo yako hunitia hekima kuliko adui zangu, Kwa maana ninayo sikuzote. Ninazo akili kuliko waalimu wangu wote, Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo. Ninao ufahamu kuliko wazee, Kwa kuwa nimeyashika mausia yako. Nimeiepusha miguu yangu na kila njia mbaya, Ili nilitii neno lako. Sikuziacha hukumu zako, Maana Wewe mwenyewe umenifundisha. Mausia yako ni matamu sana kwangu, Kupita asali kinywani mwangu. Kwa mausia yako najipatia ufahamu, Ndiyo maana naichukia kila njia ya uongo.

Soma Zaburi 119