Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Yakobo 4:5-10

Yakobo 4:5-10 SRUV

Au mwadhani ya kwamba Maandiko yasema bure? Huyo Roho akaaye ndani yetu hututamani kiasi cha kuona wivu? Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu. Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili. Huzunikeni na kuomboleza na kulia. Kucheka kwenu na kugeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa huzuni kubwa. Jidhilini mbele za Bwana, naye atawakuza.

Soma Yakobo 4

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Yakobo 4:5-10