Lk 9:1, 2, 3, 4, 5, 6, 7, 8
Lk 9:1 SUV
Akawaita wale Thenashara, akawapa uwezo na mamlaka juu ya pepo wote na kuponya maradhi.
Lk 9:3 SUV
Akawaambia, Msichukue kitu kwa safari yenu, fimbo, wala mkoba, wala mkate, wala fedha, wala mmoja wenu asiwe na kanzu mbili.
Lk 9:5 SUV
Na wale wasiowakaribisha, mtokapo katika mji huo, yakung’uteni hata mavumbi ya miguuni mwenu, kuwa ushuhuda juu yao.
Lk 9:6 SUV
Wakaenda, wakazunguka katika vijiji, wakihubiri injili, na kupoza watu kila mahali.
Lk 9:7 SUV
Na Herode mfalme akasikia habari za yote yaliyotendeka, akafadhaika kwa sababu watu wengine walisema ya kwamba Yohana amefufuka katika wafu
Lk 9:8 SUV
na wengine ya kwamba Eliya ametokea, na wengine ya kwamba mmojawapo wa manabii wa kale amefufuka.