Zaburi 75
75
Zaburi 75
Mungu ni mwamuzi
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu”. Zaburi ya Asafu. Wimbo.
1 Ee Mungu, tunakushukuru,
tunakushukuru wewe,
kwa kuwa jina lako li karibu;
watu husimulia matendo yako ya ajabu.
2 Unasema, “Ninachagua wakati maalum;
ni mimi nihukumuye kwa haki.
3 Dunia inapotetemeka na watu wake wote,
ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
4 Kwa wale wenye majivuno ninasema,
‘Msijisifu tena,’
kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
5 Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu;
msiseme kwa kiburi.’ ”
6Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi
au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye:
Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
8 Mkononi mwa Bwana kuna kikombe
kilichojaa mvinyo unaotoka povu
uliochanganywa na vikolezo;
huumimina, nao waovu wote wa dunia
hunywa hata tone la mwisho.
9 Bali mimi, nitatangaza hili milele;
nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
10 Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote,
bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 75: NEN
Kuonyesha
Nakili
Linganisha
Shirikisha
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Holy Bible, Kiswahili Contemporary Version™ (Neno: Biblia Takatifu™) | Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.
Biblica® Cross Reference System | Copyright © 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.