Zaburi 69:1-3
Zaburi 69:1-3 NEN
Ee Mungu, niokoe, kwa maana maji yamenifika shingoni. Ninazama kwenye vilindi vya matope, pasipo mahali pa kukanyaga, Nimefika kwenye maji makuu, mafuriko yamenigharikisha. Nimechoka kwa kuomba msaada, koo langu limekauka. Macho yangu yanafifia, nikimtafuta Mungu wangu.