Zaburi 48
48
Zaburi 48
Sayuni, mji wa Mwenyezi Mungu
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora.
1Mwenyezi Mungu ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana,
katika mji wa Mungu wetu,
mlima wake mtakatifu.
2Ni mzuri katika kuinuka juu kwake,
furaha ya dunia yote.
Kama vilele vya juu vya Safoni#48:2 au mlima mtakatifu au upande wa kaskazini ni Mlima Sayuni,
mji wa Mfalme Mkuu.
3Mungu yuko katika ngome zake;
amejionesha mwenyewe kuwa ngome yake.
4Wafalme walipounganisha nguvu,
waliposonga mbele pamoja,
5walimwona, wakashangaa,
wakakimbia kwa hofu.
6Kutetemeka kuliwashika huko,
maumivu kama ya mwanamke
mwenye uchungu wa kuzaa.
7Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi
zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
8Kama tulivyokuwa tumesikia,
ndivyo tulivyoona
katika mji wa Mwenyezi Mungu,
Mungu wa majeshi ya mbinguni,
katika mji wa Mungu wetu:
Mungu ataufanya uwe salama milele.
9Ee Mungu, hekaluni mwako
tunatafakari upendo wako usiokoma.
10Ee Mungu, kama jina lako lilivyo,
sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia,
mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
11Mlima Sayuni unashangilia,
vijiji vya Yuda vinafurahi
kwa sababu ya hukumu zako.
12Tembeeni katika Sayuni,
uzungukeni mji,
hesabuni minara yake;
13yatafakarini vyema maboma yake,
angalieni ngome zake,
ili mpate kusimulia habari zake
kwa kizazi kijacho.
14Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele;
atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 48: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.