Zaburi 47
47
Zaburi 47
Mtawala mwenye enzi yote
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora.
1Pigeni makofi, enyi mataifa yote,
mpigieni Mungu kelele za shangwe!
2Jinsi gani alivyo wa kutisha, Mwenyezi Mungu Aliye Juu Sana,
Mfalme mkuu juu ya dunia yote!
3Ametiisha mataifa chini yetu,
watu wengi chini ya miguu yetu.
4Alituchagulia urithi wetu,
fahari ya Yakobo, aliyempenda.
5Mungu amepaa kwa kelele za shangwe,
Mwenyezi Mungu kwa sauti za tarumbeta.
6Mwimbieni Mungu sifa, imbeni sifa,
mwimbieni sifa Mfalme wetu, imbeni sifa.
7Kwa kuwa Mungu ni mfalme wa dunia yote,
mwimbieni zaburi za sifa.
8Mungu anayatawala mataifa,
Mungu ameketi kwenye kiti chake cha enzi kitakatifu.
9Wakuu wa mataifa wanakusanyika
kama watu wa Mungu wa Ibrahimu,
kwa kuwa wafalme wa dunia ni mali ya Mungu;
yeye ametukuka sana.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 47: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.