YouVersion Logo
Search Icon

Mathayo 9:1, 2, 3, 4, 5, 6, 7, 8

Mathayo 9:1 NENO

Isa akaingia kwenye chombo, akavuka na kufika katika mji wa kwao.

Mathayo 9:2 NENO

Wakati huo huo wakamletea mtu aliyepooza, akiwa amelazwa kwenye mkeka. Isa alipoiona imani yao, alimwambia yule mtu aliyepooza, “Mwanangu, jipe moyo mkuu. Dhambi zako zimesamehewa.”

Mathayo 9:3 NENO

Kwa ajili ya jambo hili, baadhi ya walimu wa Torati wakasema mioyoni mwao, “Huyu mtu anakufuru!”

Mathayo 9:4 NENO

Lakini Isa akiyafahamu mawazo yao, akawaambia, “Kwa nini mnawaza maovu mioyoni mwenu?

Mathayo 9:5 NENO

Je, ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uende’?

Mathayo 9:6 NENO

Lakini nataka mpate kujua kwamba Mwana wa Adamu ana mamlaka duniani kusamehe dhambi.” Ndipo akamwambia yule aliyepooza, “Inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani mwako.”

Mathayo 9:7 NENO

Yule mtu akasimama, akaenda nyumbani mwake.

Mathayo 9:8 NENO

Umati wa watu walipoyaona haya, wakajawa na hofu ya Mungu, wakamtukuza Mungu aliyekuwa amewakabidhi wanadamu mamlaka kama haya.