Malaki 3:17-18
Malaki 3:17-18 NENO
“Nao watakuwa watu wangu,” asema Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni, “katika siku ile nitakapowafanya kuwa hazina yangu ya pekee. Nitawahurumia, kama vile kwa huruma mtu amhurumiavyo mwanawe anayemtumikia. Kwa mara nyingine tena utaona tofauti kati ya wenye haki na waovu, kati ya wale wanaomtumikia Mungu na wale wasiomtumikia.