YouVersion Logo
Search Icon

Luka 22:66, 67, 68, 69, 70

Luka 22:66 NENO

Kulipopambazuka, Baraza la Wazee, yaani viongozi wa makuhani na walimu wa Torati, wakakutana pamoja, naye Isa akaletwa mbele yao.

Luka 22:67 NENO

Wakamwambia, “Kama wewe ndiwe Al-Masihi, tuambie.” Isa akawajibu, “Hata nikiwaambia, hamtaamini.

Luka 22:68 NENO

Nami nikiwauliza swali, hamtanijibu.

Luka 22:69 NENO

Lakini kuanzia sasa, Mwana wa Adamu ataketi mkono wa kuume wa Mungu Mwenye Nguvu.”

Luka 22:70 NENO

Wote wakauliza, “Wewe basi ndiwe Mwana wa Mungu?” Yeye akawajibu, “Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye.”