YouVersion Logo
Search Icon

Luka 21:27, 28, 29, 30, 31, 32, 33, 34, 35, 36, 37

Luka 21:27 NENO

Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.

Luka 21:28 NENO

Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”

Luka 21:29 NENO

Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.

Luka 21:30 NENO

Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.

Luka 21:31 NENO

Vivyo hivyo, mnapoyaona mambo haya yakitukia, mtambue kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.

Luka 21:32 NENO

“Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.

Luka 21:33 NENO

Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.

Luka 21:34 NENO

“Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama mtego unasavyo.

Luka 21:35 NENO

Hivyo ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote wanaoishi katika uso wa dunia yote.

Luka 21:36 NENO

Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”

Luka 21:37 NENO

Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alienda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.

Free Reading Plans and Devotionals related to Luka 21:27, 28, 29, 30, 31, 32, 33, 34, 35, 36, 37