Yohana 7:45, 46, 47, 48, 49, 50, 51, 52
Yohana 7:45 NENO
Hatimaye wale walinzi wa Hekalu wakarudi kwa viongozi wa makuhani na Mafarisayo waliokuwa wamewatuma ili kumkamata Yesu, wakaulizwa, “Mbona hamkumkamata?”
Yohana 7:46 NENO
Wale walinzi wakajibu, “Kamwe hajanena mtu yeyote kama yeye anenavyo.”
Yohana 7:48 NENO
Je, kuna kiongozi yeyote au mmoja wa Mafarisayo ambaye amemwamini?
Yohana 7:49 NENO
Lakini umati huu wa watu wasiojua Sheria ya Musa, wamelaaniwa.”
Yohana 7:50 NENO
Ndipo Nikodemo, yule aliyekuwa amemwendea Yesu siku moja usiku, na alikuwa mmoja wao, akauliza
Yohana 7:51 NENO
“Je, sheria zetu zinaturuhusu kumhukumu mtu kabla ya kumsikiliza na kufahamu alilotenda?”
Yohana 7:52 NENO
Wakamjibu, “Je, wewe pia unatoka Galilaya? Chunguza nawe utaona kwamba hakuna nabii atokae Galilaya!” [