YouVersion Logo
Search Icon

Yohana 7:1, 2, 3, 4, 5, 6, 8, 9, 10

Yohana 7:1 NENO

Baada ya mambo haya, Isa alienda sehemu mbalimbali za Galilaya. Hakutaka kwenda Yudea kwa sababu viongozi wa Wayahudi huko walitaka kumuua.

Yohana 7:2 NENO

Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.

Yohana 7:3 NENO

Hivyo ndugu zake Isa wakamwambia, “Ondoka hapa uende Yudea ili wanafunzi Wako wapate kuona miujiza unayofanya.

Yohana 7:4 NENO

Mtu anayetaka kujulikana hafanyi mambo yake kwa siri. Kama unafanya mambo haya, jioneshe kwa ulimwengu.”

Yohana 7:5 NENO

Hata ndugu zake mwenyewe hawakumwamini.

Yohana 7:6 NENO

Isa akawaambia, “Wakati wangu bado haujawadia, lakini wakati wenu upo siku zote.

Yohana 7:8 NENO

Ninyi nendeni kwenye Sikukuu, lakini mimi sitahudhuria Sikukuu hii kwa sababu wakati wangu haujawadia.”

Yohana 7:9 NENO

Baada ya kusema hayo, akabaki Galilaya.

Yohana 7:10 NENO

Lakini ndugu zake walipokwisha kuondoka kwenda kwenye Sikukuu, yeye pia alienda lakini kwa siri.