Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Yeremia 31:33-34

Yeremia 31:33-34 NEN

“Hili ndilo agano nitakalofanya na nyumba ya Israeli baada ya siku zile,” asema BWANA. “Nitaweka sheria yangu katika nia zao, na kuiandika mioyoni mwao. Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Mtu hatamfundisha tena jirani yake, wala mtu kumfundisha ndugu yake akisema, ‘Mjue BWANA Mungu,’ kwa sababu wote watanijua mimi, tangu aliye mdogo kabisa kwao, hadi aliye mkuu sana,” asema BWANA. “Kwa sababu nitasamehe uovu wao, wala sitazikumbuka dhambi zao tena.”