Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Isaya 40:1-5

Isaya 40:1-5 NEN

Wafarijini, wafarijini watu wangu, asema Mungu wenu. Sema na Yerusalemu kwa upole, umtangazie kwamba kazi yake ngumu imekamilika, kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia, kwamba amepokea kutoka mkononi mwa BWANA maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote. Sauti ya mtu aliaye: “Itengenezeni jangwani njia ya BWANA, nyoosheni njia kuu nyikani kwa ajili ya Mungu wetu. Kila bonde litainuliwa, kila mlima na kilima kitashushwa; penye mabonde patanyooshwa, napo palipoparuza patasawazishwa. Utukufu wa BWANA utafunuliwa, nao wanadamu wote watauona pamoja. Kwa maana kinywa cha BWANA kimenena.”