Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Kumbukumbu 8:11-15

Kumbukumbu 8:11-15 NEN

Jihadharini msimsahau BWANA Mungu wenu, mkashindwa kushika maagizo yake, sheria na amri zake ambazo ninawapa leo. Angalia wakati mtakapokuwa mmekula na kushiba, mkajenga nyumba nzuri na kukaa humo, na wakati makundi yenu ya ngʼombe na mbuzi na kondoo yatakapoongezeka na fedha na dhahabu yenu itakapoongezeka na vyote mlivyo navyo vitakapozidishwa, basi mioyo yenu isiwe na kiburi mkamsahau BWANA Mungu wenu aliyewatoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa. Aliwaongoza kupitia jangwa lile kubwa na la kutisha, nchi ile ya kiu isiyo na maji, yenye nyoka wa sumu na nge. Aliwatolea maji kutoka kwenye mwamba mgumu.

Video for Kumbukumbu 8:11-15