Ole wao wale wanaoshuka Misri kutafuta msaada,
wale wanaotegemea farasi,
wanaoweka tumaini katika wingi wa magari yao ya vita,
na katika nguvu nyingi za wapanda farasi,
lakini hawamwangalii yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli,
wala hawatafuti msaada kwa Mwenyezi Mungu.