1
Mhubiri 11:9
Neno: Maandiko Matakatifu 2024
Furahi ewe kijana, ukiwa bado kijana, moyo wako na ukupe furaha siku za ujana wako. Fuata njia za moyo wako na chochote macho yako yanaona, lakini ujue kwamba kwa ajili ya haya yote Mungu atakuleta hukumuni.
Linganisha
Chunguza Mhubiri 11:9
2
Mhubiri 11:10
Kwa hiyo, ondoa wasiwasi moyoni mwako na utupilie mbali masumbufu ya mwili wako, kwa kuwa ujana na nguvu ni ubatili.
Chunguza Mhubiri 11:10
3
Mhubiri 11:4
Yeyote atazamaye upepo hatapanda, yeyote anayeangalia mawingu hatavuna.
Chunguza Mhubiri 11:4
4
Mhubiri 11:5
Kama vile usivyofahamu njia ya upepo, au jinsi mwili uumbwavyo ndani ya tumbo la mama, vivyo hivyo huwezi kufahamu kazi ya Mungu, Muumba wa vitu vyote.
Chunguza Mhubiri 11:5
5
Mhubiri 11:6
Panda mbegu yako asubuhi, nako jioni usiruhusu mikono yako ilegee, kwa maana hujui ni ipi itakayofanikiwa, kwamba ni hii au ni ile, au kwamba zote zitafanikiwa sawasawa.
Chunguza Mhubiri 11:6
6
Mhubiri 11:2
Wape sehemu watu saba, naam hata wanane, kwa maana hujui ni baa gani litakalokuwa juu ya nchi.
Chunguza Mhubiri 11:2
Nyumbani
Bibilia
Mipango
Video