Maneno ya Amosi, mmoja wa wachungaji wa Tekoa: yale aliyoyaona kuhusu Israeli miaka miwili kabla ya tetemeko la ardhi, wakati Uzia alikuwa mfalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yehoashi alikuwa mfalme wa Israeli.
Alisema:
“Mwenyezi Mungu ananguruma toka Sayuni,
pia ananguruma kutoka Yerusalemu;
malisho ya wachungaji yanakauka,
kilele cha Karmeli kinanyauka.”