Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Flp 2:9

Kupata Uhuru kutokana na Kufadhaika
Siku 5
Kufadhaika huwa, lakini hakufai kuyaendesha maisha yako. Kumpitia Kristo, tunaweza kuibadilisha, kuiona upya na kuitafsiri upya. Kama unapata changamoto na kufadhaika, angalia mpango huu wa Bibilia wa siku 5 ili ujifunze kupata uhuru na amani.

Mwanamume Wa Kifalme
Siku 5
Katika historia yote, Mungu daima amewatafuta na kuwatumia wanaume kuendeleza ajenda ya Ufalme wake. Shetani anajua hili, ndiyo maana anataka kuwafungia na kuwahasi wanaume. Ulimwengu wetu unaendelea ukizorota kwa sababu wanaume hawapatikani popote. Ni wakati wa wanaume kusimama kidete. Katika mpango huu wa kusoma wa siku tano, Daktari Tony Evans atakupeleka kwenye safari ya kufanyika mwanamume ambaye Mungu alikuumba uwe.

Nenda Tenda Sema Toa: Uhuru wa Kujisalimisha kwa Yesu
Siku 7
Kujisalimisha kwa Yesu ni tukio kubwa maishani. Lakini uamuzi huu unamaanisha nini na tutauishi vipi kila siku? Uamuzi ni wa mambo makubwa ya maisha pekee, ama wacha Mungu kupita kiasi? Woga, makosa yaliyopita, na kutoelewa vinaweza kutuzuia. "Nenda Tenda Sema Toa" ni ahadi/sala ambayo inafunua jinsi utakavyochukua hatua zinazofuata katika safari yako ya kiroho. Pata uhuru unaotokana na kumfuata Yesu.

Msalaba Na Pasaka
Siku 7
Tunavaa misalaba shingoni mwetu, lakini tunapaswa kuitumiaje kwa maisha yetu? Kazi ya Yesu ina nguvu ya ajabu kwetu. Bila Ijumaa, hakungekuwa na Jumapili. Pasaka isingetokea bila msalaba. Gundua jinsi msalaba unavyounganamanisha katika maisha yako kupitia mpango huu wa usomaji wa ibada unapotayarisha moyo wako kwa Pasaka.

Soma Biblia Kila Siku Juni/2022
Siku 30
Soma Biblia Kila Siku Juni/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Juni pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa siku husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Wafilipi na Mwanzo. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure