Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Mwa 1:26
![Mwanamume Wa Kifalme](/_next/image?url=https%3A%2F%2F%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F35208%2F640x360.jpg&w=1920&q=75)
Mwanamume Wa Kifalme
Siku 5
Katika historia yote, Mungu daima amewatafuta na kuwatumia wanaume kuendeleza ajenda ya Ufalme wake. Shetani anajua hili, ndiyo maana anataka kuwafungia na kuwahasi wanaume. Ulimwengu wetu unaendelea ukizorota kwa sababu wanaume hawapatikani popote. Ni wakati wa wanaume kusimama kidete. Katika mpango huu wa kusoma wa siku tano, Daktari Tony Evans atakupeleka kwenye safari ya kufanyika mwanamume ambaye Mungu alikuumba uwe.
![Ndoa Ya Ufalme](/_next/image?url=https%3A%2F%2F%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F35246%2F640x360.jpg&w=1920&q=75)
Ndoa Ya Ufalme
Siku 5
Ndoa huja na furaha nyingi na changamoto kubwa. Sababu mojawapo ya changamoto hizo ni kwa sababu tumesahau kusudi la kibiblia la ndoa. Tumemuondoa Mungu na kufafanua ndoa kwa msingi ya furaha. Lakini ndoa ipo ili kumtukuza Mungu kwa kupanua wigo Wake ulimwenguni kote. Katika mpango huu wa siku tano wa kusoma, Dkt. Tony Evans anakupeleka kwenye safari ya ndoa ya ufalme.
![Tabia](/_next/image?url=https%3A%2F%2F%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F13743%2F640x360.jpg&w=1920&q=75)
Tabia
SIku 6
Mabadiliko si rahisi, lakini si kwamba hayawezekani. Kuanza tabia chache rahisi itabadilisha jinsi unajiona leo na kukugeuza uwe mtu ambaye ungependa kuwa kesho. Mpango huu wa Biblia wa Life.Church unatazama Maandiko ili kutengeneza tabia za kila siku ambazo zitadumu.
![Kutaka](/_next/image?url=https%3A%2F%2F%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F9245%2F640x360.jpg&w=1920&q=75)
Kutaka
Siku 7
Katika siku hizi 7 za kusoma na kujifunza, Beth Moore anatumia maswali kutoka katika Maandiko Matakatifu ili kukuongoza kwenye uhusiano wa ndani zaidi na Yeye anayekujua vizuri. Alama za uandishi zilizopotoka mwisho wa sentensi zinaonyesha udadisi, hamu au labda wasiwasi. Swali ni mwaliko toka katika hali hatarishi hadi ukaribu wa ndani zaidi. Biblia haiachi ukaribisho huo. Mara kwa mara tunaona watu wa Mungu wakimuuliza Muumbaji wao maswali. Na pia tunamwona Mungu Muumbaji akiuliza maswali kwa viumbe wake. Changamoto ni kupokea mwaliko. Jifunze kuchimba ndani ya Neno la Mungu, kujibu maswali ya Mungu, na kuleta maswali mbele Zake. Ruhusu alama za uandishi zilizopotoka ziwe ramani ya kusogeza uhusiano wako na Baba yako kuwa wa ukaribu zaidi.
![Yesu Ananipenda](/_next/image?url=https%3A%2F%2F%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F23705%2F640x360.jpg&w=1920&q=75)
Yesu Ananipenda
Siku 7
Ikiwa mtu angekuuliza, "Ninahitaji kuamini ipi ili niwe Mkristo?" ungemjibu vipi? Kwa kutumia maneno ya wimbo upendwao, "Yesu anipenda, kweli ninajua, kwani Biblia inasema”, mhubiri aliyekuwa mwanahabari anakusaidia kuelewa unachoamini na sababu. Mwandishi maarufu John S. Dickerson anafafanua imani za kimsingi za Kikristo kwa uwazi na uaminifu na kuashiria mbona imani hizi ni muhimu.