Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Efe 6:11
![Mpango wa kupigana Vita vya Kiroho](/_next/image?url=https%3A%2F%2F%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F9220%2F640x360.jpg&w=1920&q=75)
Mpango wa kupigana Vita vya Kiroho
Siku 5
Kwa haya mafundisho ya nguvu utaelewa kwa kina kuhusu jinsi ya kutengeneza njia ya kumpita adui na kuzuia mpango wake wa kuharibu maisha yako
![Naweza Kweli Kushinda Dhambi na Majaribu?](/_next/image?url=https%3A%2F%2F%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F20280%2F640x360.jpg&w=1920&q=75)
Naweza Kweli Kushinda Dhambi na Majaribu?
Siku 5
Umewahi kujiuliza, “Mbona bado napambana na dhambi hiyo?” Hata mtume Paulo alisema hivyo katika Warumi 7:15: “ Sifanyi ninachotaka, lakini nafanya kile ninachochukia.” Je, tunazuiaje dhambi kusimamisha maisha yetu ya kiroho? Je, hata inawezekana? Hebu tujadili dhambi, majaribu, Shetani, na, kwa shukrani, upendo wa Mungu.
![Silaha ya Mungu](/_next/image?url=https%3A%2F%2F%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F25281%2F640x360.jpg&w=1920&q=75)
Silaha ya Mungu
Siku 5
Kila siku, vita isiyoonekana inapiganwa kukuzunguka--haionekani, haisikiki, lakini bado unaihisi katika maisha yako yote. Adui wa kishetani aliyejitoa kuleta uharibifu kwa kila kitu muhimu kwako: moyo wako, akili yako, ndoa yako, watoto wako, ndoto zako, hatima yako. Lakini mpango wake wa vita unategemea kukustukiza wakati huna silaha za vita. Kama umechoka kusukumwa na kusitukizwa, somo hili ni kwa ajili yako.
![Ndoa Ya Ufalme](/_next/image?url=https%3A%2F%2F%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F35246%2F640x360.jpg&w=1920&q=75)
Ndoa Ya Ufalme
Siku 5
Ndoa huja na furaha nyingi na changamoto kubwa. Sababu mojawapo ya changamoto hizo ni kwa sababu tumesahau kusudi la kibiblia la ndoa. Tumemuondoa Mungu na kufafanua ndoa kwa msingi ya furaha. Lakini ndoa ipo ili kumtukuza Mungu kwa kupanua wigo Wake ulimwenguni kote. Katika mpango huu wa siku tano wa kusoma, Dkt. Tony Evans anakupeleka kwenye safari ya ndoa ya ufalme.
![Kutaka](/_next/image?url=https%3A%2F%2F%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F9245%2F640x360.jpg&w=1920&q=75)
Kutaka
Siku 7
Katika siku hizi 7 za kusoma na kujifunza, Beth Moore anatumia maswali kutoka katika Maandiko Matakatifu ili kukuongoza kwenye uhusiano wa ndani zaidi na Yeye anayekujua vizuri. Alama za uandishi zilizopotoka mwisho wa sentensi zinaonyesha udadisi, hamu au labda wasiwasi. Swali ni mwaliko toka katika hali hatarishi hadi ukaribu wa ndani zaidi. Biblia haiachi ukaribisho huo. Mara kwa mara tunaona watu wa Mungu wakimuuliza Muumbaji wao maswali. Na pia tunamwona Mungu Muumbaji akiuliza maswali kwa viumbe wake. Changamoto ni kupokea mwaliko. Jifunze kuchimba ndani ya Neno la Mungu, kujibu maswali ya Mungu, na kuleta maswali mbele Zake. Ruhusu alama za uandishi zilizopotoka ziwe ramani ya kusogeza uhusiano wako na Baba yako kuwa wa ukaribu zaidi.
![Yesu: Bendera Wetu wa Ushindi](/_next/image?url=https%3A%2F%2F%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F14894%2F640x360.jpg&w=1920&q=75)
Yesu: Bendera Wetu wa Ushindi
Siku 7
Tunapo sherehekea Pasaka, tunasherehekea ushindi mkuu katika historia. Kupitia kifo cha Yesu na kufufuka, alishinda nguvu ya dhambi na kaburi, na athari zake zote, na alichagua kushiriki ushindi huo nasi. Pasaka hii, hebu tuangalie baadhi ya ngome alizozishinda, angalia vita alivyovipiga kwa ajili yetu, na umsifu kama bendera ya ushindi wetu.
![Soma Biblia Kila Siku Februari/ 2022](/_next/image?url=https%3A%2F%2F%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F29872%2F640x360.jpg&w=1920&q=75)
Soma Biblia Kila Siku Februari/ 2022
siku 28
Soma Biblia Kila Siku Februari/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Februari pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa situ husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Waefeso. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure.
![Jolt ya Furaha](/_next/image?url=https%3A%2F%2F%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F228%2F640x360.jpg&w=1920&q=75)
Jolt ya Furaha
Siku 31
Biblia inatuambia kwamba "Katika uwepo wake kuna furaha tele" na kuwa "furaha ya Bwana ni nguvu yetu". Furaha sio hisia tu bali ni tunda la Roho na mojawapo ya silaha bora katika gala letu la kupigana na kuvunjika moyo, huzuni na kushindwa. Tumia siku 31 ukijifunza ni nini Biblia inasema kuhusu Furaha na kujiimarisha kuwa Mkristo mwenye Furaha bila wasi wasi.