Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na 1 Kor 13:7

Upendo na Ndoa
Siku 5
Kwa kuangazia ndoa yetu ndani ya muktadha wa Maandiko, tunampa Mungu fursa ya kufichua maarifa mapya kuhusu uhusiano wetu na kuimarisha kifungo chetu. Mpango huu unaangazia kifungu kilicholenga cha Maandiko na mawazo ya haraka kila siku ili kuanzisha majadiliano na maombi na mwenzi wako. Mpango huu wa siku tano ni ahadi ya muda mfupi ya kukusaidia kuwekeza katika uhusiano wako wa maisha. Kwa maudhui zaidi, angalia finds.life.church

Hekima Kamilifu: Safari ya Siku 7 ya akina Baba
Siku 7
Inashangaza kiasi ambacho baba zetu wanatufinyanga. Hakuna mtu anayeepuka nguvu na mvuto wa baba yao wa kidunia. Na kwa sababu wanaume wengi wanahisi kuwa hawako tayari kuwa baba, ni muhimu kutafuta mwongozo – kwenye Maandiko na kutoka kwa baba wengine. Hekima Kamilifu ni safari kuelekea hekima na busara kwa kina baba, inayohusisha kanuni na hekima kutoka kwenye Maandiko pamoja na uzoefu wa baba mwenye umri mkubwa na hekima zaidi ambaye amejifunza kutokana na makosa yake.

Ibada juu ya Vita vya Akilini
Siku 14
Hii ibada itakusaidia kwa himizo za tumaini la kushinda hasira, machafuko, hukumu, hofu, shaka ... chochote kile. Ufahamu huu utakusaidia kujua njama ya adui ya kukuchanganya na kukudanganya, kukabiliana na mwelekeo wa mawazo ulioharibika, kupata ushindi katika kubadilisha mawazo yako, kupata nguvu, kutiwa moyo na, muhimu zaidi, ushindi juu ya kila vita akilini mwako. Una nguvu ya kupigana ... hata ikiwa ni siku moja kwa wakati!

BibleProject | Tafakari ya Ujio wa Yesu
Siku 28
BibleProject ilibuni Tafakari ya Ujio wa Yesu ili kuhamasisha watu mmoja mmoja, vikundi vidogo vidogo, na familia kusherehekea majilio, au kuwasili kwa Yesu. Mwongozo huu wa wiki nne unashirikisha video za kikatuni, mihutasari mifupi, na maswali ya kutafakari ili kuwasaidia washiriki kuchunguza maana ya Biblia ya tumaini, amani, furaha, na upendo. Chagua mwongozo huu ili kujifunza jinsi maadili haya manne yamefika ulimwenguni kupitia kwa Yesu.