1
Yohana 6:35
Swahili Roehl Bible 1937
Yesu akawaambia: Mimi ndio mkate wa uzima; ajaye kwangu hataona njaa, naye anitegemeaye hataona kiu hata siku moja.
Yenzanisa
Ongorora {{vhesi}}
2
Yohana 6:63
Roho ndiyo inayotupatia uzima, mwili haufai kitu. Maneno, niliyowaambia, ndiyo ya Kiroho yenye uzima.
3
Yohana 6:27
Sumbukieni vyakula! Lakini vile vinavyoangamia sivyo, ni vile vinavyokaa, viwafikishe penye uzima wa kale na kale, navyo ndivyo, Mwana wa mtu atakavyowapani ninyi. Kwani huyu ndiye, Baba Mungu aliyemwagiza hivyo na kumtia muhuri.
4
Yohana 6:40
Kwani haya ndiyo mapenzi ya Baba yangu: kila anayemtazamia Mwana na kumtegemea apate uzima wa kale na kale, nami nitamfufua siku ya mwisho.
5
Yohana 6:29
Yesu akajibu, akawaambia: Hii ndiyo kazi ya Mungu, mkimtegemea yeye, aliyemtuma.*
6
Yohana 6:37
Wote, Baba anipao, ndio watakaokuja kwangu; naye ajaye kwangu sitamfukuza, ajiendee.
7
Yohana 6:68
ndipo, Simoni Petero alipomjibu: Bwana, tumwendee nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa kale na kale.
8
Yohana 6:51
Mimi ndio mkate wenye uzima ulioshuka toka mbinguni. Mtu atakayeula mkate huu atakuwa mzima pasipo mwisho. Nao mkate, nitakaowapa mimi, ndio mwili wangu utakaotolewa, ulimwengu upate uzima.
9
Yohana 6:44
Hakuna awezaye kuja kwangu, Baba aliyenituma asipomvuta, nami nitamfufua siku ya mwisho.
10
Yohana 6:33
Kwani mkate wa Mungu ndio ule ushukao toka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.
11
Yohana 6:48
Mimi ndio mkate wa uzima.
12
Yohana 6:11-12
Kisha Yesu akaitwaa ile mikate, akashukuru, akawagawia waliokaa; vile vile navyo visamaki, kama walivyotaka. Lakini waliposhiba, akawaambia wanafunzi wake: Yakusanyeni makombo yaliyosalia, pasipatikane kinachopotea!
13
Yohana 6:19-20
Walipokwisha endelea mwendo wa nusu saa na kupita kidogo, wakamwona Yesu, anavyokwenda juu ya bahari na kukifikia chombo karibu, wakaogopa. Ndipo, alipowaambia: Ni miye, msiogope!
Pekutangira
Bhaibheri
Zvirongwa
Mavideo