1
Mwanzo 9:12-13
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
Tena Mungu akasema: “Hiki ndicho kitambulisho cha agano ninalofanya kati yangu nanyi na kila kiumbe chenye uzima kinachokuwa pamoja nanyi kwa vizazi vyote vinavyokuja: ninaweka upinde wangu katika mawingu, nao utakuwa kitambulisho cha agano kati yangu na dunia.
Yenzanisa
Ongorora {{vhesi}}
2
Mwanzo 9:16
Huo upinde utakapotokea katika mawingu, nitauona na kukumbuka agano hilo la milele kati yangu na viumbe vyote vyenye uzima katika dunia.”
3
Mwanzo 9:6
Anayemwanga damu ya mwanadamu, damu yake itamwangwa na mwanadamu; maana mwanadamu aliumbwa kwa mufano wa Mungu.
4
Mwanzo 9:1
Mungu akamubariki Noa na wana wake, akiwaambia: “Muzae, muongezeke, mujaze inchi.
5
Mwanzo 9:3
Nyama wote wenye uzima watakuwa chakula chenu; ninawapa nyama hao kama vile nilivyowapa mimea kuwa chakula chenu.
6
Mwanzo 9:2
Nyama wote, ndege wote wa anga, viumbe vyote vinavyotambaa juu ya inchi na samaki wote wa bahari watakuwa na hofu na kuwaogopa ninyi. Wote wamewekwa chini ya mamlaka yenu.
7
Mwanzo 9:7
Nanyi muzae, mwongezeke, muzae kwa wingi, mwongezeke katika inchi.”
Pekutangira
Bhaibheri
Zvirongwa
Mavideo